Unknown Unknown Author
Title: MOJA KWA MOJA:Manchester City dhidi ya Leicester
Author: Unknown
Rating 5 of 5 Des:
Mechi kati ya viongozi wa ligi ya Uingereza Leicester City dhidi ya Manchester City ambao wako katika nafasi ya pili katika jedwali la ligi...
Mechi kati ya viongozi wa ligi ya Uingereza Leicester City dhidi ya Manchester City ambao wako katika nafasi ya pili katika jedwali la ligi hiyo17.38pm:Na Mechi inakamilika hapa Leicester City wakiibuka kidedea kwa bao 3-1 dhidi ya wenyeji Manchester City.
17.37pm:Lalalal Manchester City wakosa bao la wazi hapa baada ya gusa niguse ya Aguero na Fernando
17.36pm:Baada ya kupata bao la kwanza wachezaji wa Manchester City wanajaribu kila njia hapa kupata bao la pili
Aguero
17.30pm:Goooooooooooal Aguero aipatia Manchester City bao la kufutia machozi
17.27pm:Mashabiki wa manchester City wanaonekana wakiondoka katika uwanja wao wa Etihad kufuatia mvua hiyo ya mabao
17.26pm: Safu ya mashambulizi ya Manchester City imeshindwa kabisa kuivunja safu ya ulinzi ya Leicester.
17.24pm: Lalalala Verdy akosa bao la nne hapa.Ama kwa kweli ni mvua inyowanyeshea Manchester City
17.21pm:Mahrez naye anatoka kwa upande wa Leicester City
  • Gor Mahia imelazwa na Bandari 1-0 katika mechi ya kombe la Gotv mjini Mombasa, kenya
17.20Pm:David Silva atolewa na badala yake Saligno aingia
Kocha wa Leicester Claudio Ranieri
17.18pm:Hali si hali hapa katika uwanja wa Etihad nchini Uingereza ambapo mabingwa wa zamani wa ligi ya Uingereza Manchester City wameadhibiwa bao tatu bila jibu.
Bao leicester
17.07pm:Goooooooooooal Leicester City yajipatia bao la tatu dhidi ya Manchester City hapa.Amini usiamini vijana wa Claudio Ranieri wanatamba kama ambaye hawako Etihad
16.57pm:La.la.la.la Manchester City wakosa bao hapa kunako dakika tisa lakini kipa anaukoa.
16.54pm:Wachezaji wa Manchester City hawaamini hapa .Inawabidi kufanya mabadiliko farbian Delph anatoka na badala yake anaingia Fernandinho.
Mahrez
16.52pm:Gooooooooooal Mahrez wa leicester City aiongezea bao la pili timu yake hapa dakika ya nne baada ya kuanza kwa kipindi cha pili
16.49pm:Na Kipindi cha pili cha mchezo kinaanza hapa katika uwanja wa Etihad.
16.34pm:Na kipindi cha kwanza cha mechi kinakamilika hapa ikiwa wenyeji manchester City wako nyuma kwa bao moja dhidi ya viongozi wa Ligi kwa sasa Leicester City.
Rahim Sterking
16.33pm:Ama kwa kweli wachezaji hawa wa manchester City wanajaribu kuona lango la wapinzani wao lakini safu ya ulinzi ya Leicester inakaa.
16.32pm:Mechi imekuwa ngumu hapa kwa upande wa Leicester ambao wamerudi nyuma kulinda lango lao.
16.31pm:Dakika za lala salama kpindi cha kwanza, Kolarov anakosa bao hapa
Aguero
16.30pm:Manchester City inatafuta bao hapa kwa udi na uvumba lakini bahati haijasimama
16.00pm:Ni Mechi inayochezwa huku kukiwa na marasha rasha ya mvua.
15.53pm:Leicester wakosa bao la pili hapa dhidi ya Mancity.
15.50pm:Manchester City Watafuta kusawazisha lakini Aguero ashindwa kuipita safu ya ulinzi ya Leicester.
Leceister
15.48pm:Goooooooal Leicester City yajipatia bao la kwanza hapa baada mkwaju wa mpira wa adhabu kupigwa,dakika tatu baada ya kuanza kwa mechi
15.45pm: Manchester City vs Leicester City. Mechi inaanza
Kikosi cha Leicester
Kikosi cha Man City




About Author

Advertisement

Post a Comment Blogger

 
Top