![]() |
| Zaidi ya watu 90 wauawa Myanmar |
Idadi ya watu waliokufa kutokana na maporomoko ya udongo katika eneo la Jade nchini myanmar imeongezeka hadi takriban watu 90.
Watu
kadha bado hawajulikani waliko. Afisa mmoja katika jimbo la kaskazini
la Kachin anasema kuwa wakoaji wanaendelea kupata maiti zaidi.Waathiriwa walifunikwa wakati mlima wa taka iliyorundikwa na makampuni ya kuchimba migodi ulipoporomoka.
Watu eneo hilo wanasema kuwa wengi wa waliouawa ni wazoaji taka wanaoishi karibu na eno hilo ambao hutafuta vifaa kwenye taka kwenda kuuza.
Ajali hiyo ilitokea mapema wakati wengi walikuw bado wamelala.

Post a Comment Blogger Facebook