12.30:Katika
kituo cha Meko, nje kidogo ya mji wa Mwanza, kumetokea sokomoko, baadhi
ya wakazi wanalalamika kwamba majina yao hayaonekani kwenye daftari la
wapiga kura.
 |
|
Seif Sharif Hamad
|
11.30am:Mgombea wa Urais kupitia chama cha upinzani CUF, Seif Sharif Hamad amepiga kura katika kisiwa kilichopo kisiwani Unguja.
 |
|
Madereva waliokosa fursa ya kupiga kura
|
11.00am:Baadhi ya wapiga kura waliojisajili katika
maeneo mengine ya bara wamelazimika kusafiri hadi maeneo hayo ili kupiga
kura.Madereva ambao hawakupewa siku ya mapumziko hawafurahii kwamba
wasingeweza kushiriki katika shughuli hiyo.
 |
| Maguful |
10.37am:Mgombea wa Urais kupitia chama cha CCM John Pombe Magufuli amepiga kura katika mkoa wa Kagera huko Chato
Ametoa
wito kwa raia wa Tanzania kujitokeza kwa wingi ili kuwachagua viongozi
wanaowahitaji.Aidha amewataka raia hao kumtanguliza mungu na kuweka
amani.
Anasema kuwa alipopiga kura mvua ilianza kunyesha akisema kuwa ni ishara ya baraka.
 |
| Taifa la Ivory Cost |
10.15am:Taifa la Ivory Coast linashiriki katika
uchaguzi mkuu ulio na ushindani mkubwa ,ikiwa ni wa kwanza kabisa tangu
kuisha kwa vita vya wenyewe kwa wenyewe mwaka 2011.Uchaguzi huo
umeathirika baada ya wagombea maarufu wa chama cha Upinzani kujiondoa
wakidai udanganyifu.
 |
| Lowassa |
10.00am:Mgombea wa Urais wa chama cha UKAWA Edward Lowassa ameandamana na mkewe katika kituo cha Arusha na kupiga kura
 |
| Wanahakiki majina kabla ya kupiga kura
|
9.39am:Wakaazi wa Unguja, visiwani Zanzibar, wakihakiki majina, kabla ya kupiga kura.
 |
| Dr. Shein |
9.36am:Mgombea wa Rais wa CCM, Zanzibar, Dokta Ali
Mohammed Shein, akiwa katika chumba cha kupiga kura, kusini Unguja.Shein
amewataka raia kujitokza kwa wingi ili kushiriki katika shughuli hiyo
ya kihistoria.
 |
| Milolongo mirefu yashuhudiwa
|
8.36am:Takriban wapiga kura milioni 22,750,789 wanashiriki katika shughuli hiyo.
 |
| Mahame |
7.50am:Huku shughuli ya upigaji kura ikiendelea maeneo
mengi yamesalia kuwa mahame zikiwemo barabara na maeneo mengi ya mji wa
Dar es Salaam.Hii ni kwa sababu raia wengi wanashiriki katika shughuli
hiyo.
 |
| Amepiga kura |
7.14am:Katika kituo cha Dodoma foleni ndefu
imeshuhudiwa ,ni kituo kilichopo katikati ya mji.Baadhi ya wapiga kura
waliofika kituoni humo na kupiga kura wanasema hakuna tatizo lolote
walilopata.
 |
| Masanduku yanayotumika kupigia kura Tanzania
|
7.13am:Katika kituo cha kinondondoni tayari watu
wameanza kupiga kura bila matatizo yoyote.Sheria ya mita 200 inaonekana
kuanza kuheshimiwa kwani watu wanapiga kura na kuondoka vituoni
7.05am:Mtafarufuku
umetokeo katika kituo cha masaki baada ya maafisa wa uchaguzi kutoka
nje ya vituo vya kupiga kura na kuwaelezea raia kupanga mistari mitatu
inayowapendelea wanawake,na wazee.Wengi wa wale waliofika mapema
wamepinga hatua hiyo wakidai kwamba ni haki yao kupiga kura wa kwanza.
 |
| WApiga kura |
7.00am:Ni saa moja kamili saa za Afrika mashariki na wakati muhimu kwa taifa la Tanzania ambapo shughuli ya upigaji kura inaanza rasmi
 |
| Waangalizi |
6.30am:Waangalizi wa kimataifa tayari wamefika
katika vituo vya kupigia kura katika maeneo mbalimbali nchini Tanzania
ili kushuhudia matukio ya uchaguzi huo.
6.30am: Ili kutaka kufahamu iwapo jina lako liko katika sajili ya uchaguzi wengi wamekuwa wakipiga nambari hizi *152*00#
Post a Comment Blogger Facebook