![]() |
| Dogo |
Najua kuna wafuatiliaji wa stori za Hekaheka kwenye show ya Leo Tena
@Clouds FM… ya leo ni mwendelezo wa kisa cha siku nyingi ambacho
kiliwahi kusikika kuhusu ishu ya mwanamke mmoja ambaye alimuuza mtoto
wake mdogo kwa Shilingi laki mmoja.
Bibi ya mtoto huyo amesikika leo kwenye
Hekaheka, amesimulia kisa chote kilivyokuwa baada ya mtoto kupatikana
amesema mtoto aliumwa sana baada ya kupatikana.
Geah Habib
kaongea pia na mtoto huyo ambaye kwa sasa amekua mkubwa, ana miaka nane
na anasoma darasa la kwanza, jina lake anaitwa Fatuma Masai kwa sababu
baada ya kuzaliwa aliuzwa laki moja kwa jamaa mmoja ambae kabila lake ni
mmasai.

Post a Comment Blogger Facebook