 |
|
Nyama ya ngombe ni haramu maeneo mengi ya India ambapo Wahindu wanaamini mnyama huyo ni 'mtakatifu'.
|
Polisi nchini India wamewatia mbaroni watu sita baada ya mwanamume mmoja
Muislamu kupigwa hadi kufa kufuatia uvumi kuwa familia yake imeficha
nyama nyumbani kwao.
 |
|
Watu 6 wamekamatwa na polisi nchini India baada ya
kumvamia na kumpiga mwanaume mmoja hadi kufa eti alikuwa amekula nyama
ya ngombe.
|
Mohammed Akhlaq alikokotwa kutoka nyumbani kwake Kaskazini mwa Uttar Pradesh na kushambuliwa na umati wa watu.
Mwanawe pia alijeruhiwa vibaya.
 |
|
Jamaa ya muathiriwa wakiomboleza kifo chake
|
Kuchinja ngombe ni haramu maeneo mengi ya India ambapo wakaazi wake wengi ni Wahindu wanaoamini mnyama huyo ni mtakatifu.
Hivi
majuzi Serikali ya chama cha Wahindu chenye mrengo wa kulia kimeweka
sheria kali zinazopiga marufuku uchinjaji wa ngombe, uuzaji wa nyama na
ulaji wake.
Post a Comment Blogger Facebook